Asili ya maua haya ni Ulaya ya magharibi, ya kati na ya kaskazini.
Mmea wenye maua haya huwa na mizizi midogo inayomea ardhini lakini si kwa kuchimba sana ndani. Mmea wa maua haya una matawi madogo ya mviringo au matawi yenye kufanana kijiko yenye refi wa sentimita 2-5, ambayo hupatikana karibu sana na ardhi. Maua yenyewe ni sentimita 2-3 kwa upana yakiwa na sehemu nyeupe iliyozunguka sehemu nyingine ya samawati;kibibimlima ni daikoti.
Kibibimlima haathiriki na ukataji wa nyasi kwa hivyo yeye huwa kama mmea haribifu bustanini, ingawa wachache hupenda umbo la maua haya. Kuna aina za kibibimlima zinazopandwa kwa ajili ya kuuza, zenye maua makubwa zaidi yenye petali zenye upana wa sentimita 5-6
Ua linatumika kimatibabu kwa sababu ya sifa zake za kufanya tishu za mwili kuwa ndogo.[1] Katika Roma ya kale, madaktari wa upasuaji waliofuata majeshi vitani waliwaamuru watumwa kukusanya magunia ya kibibimlima ili kupata kutoa maji kutoka maua yale.
Kibibimlima kimetumika tangu jadi kutengeneza vifaa vya kuremebsha katika michezo ya watoto.[2]
Asili ya maua haya ni Ulaya ya magharibi, ya kati na ya kaskazini.